FAHAMU UMUHIMU WA LISHE YA UYOGA MWILINI






Na James Zakayo

Moja ya vyakula muhimu sana katika mwili wa binadamu, vinavyoupa mwili nguvu na virutubisho vingi vya kujenga mwili ni pamoja na chakula kijulikanacho kwa jina la uyoga.

Uyoga umetajwa na baadhi ya watalaamu mbalimbali wa tiba lishe kutoka ndani na nje ya nchi juu ya faida yake kwenye suala zima la afya ikiwa ni pamoja na kuondoa sili mfu zilizoko mwilini.

Moja ya watalaam hao ni Dk. George Pamplona mwandishi wa kitabu cha Health food, moja ya tafiti zake alizoandika katika kitabu hicho anasema kuwa uyoga ni moja ya chakula maarufu sana na kinapendwa na idadi kubwa sana ya watu hasa katika kutibu ugonjwa wa kisukari.

Katika moja ya nukuu yake kwenye hicho kitabu anasema kuwa “uyoga una wingi wa protini na wingi wa vitamini kundi B ambavyo ni muhimu sana kwenye mwili kwa kuzuia na kuondoa kesi za kisukari mwilini, na husaidia kongosho katika kuzalisha kiwango sahihi cha insulini mwilini kupambana na kisukari” alifafanua.

Akiendelea kufafanua anasema kuwa uyoga utafaa kwa watu wenye kisukari ikiwa utapikwa na kuliwa bila kuwekwa mafuta , uliwe katika hali ya kutokuchangwanywa na mafuta aina yoyote ndipo utakapo kuwa na tija katika mwili na kuondoa kisukari na kuzuia.

Naye mtalaam wa tiba lishe Dk. Raphael Nyampiga kutoka kliniki ya Atukuzwe iliyoko Pugu jijini Dar es salaam anasema kuwa uyoga ni maarufu sana kwa watanzania kila jamii nchini inafahamu chakula hiki kizuri japo wengi wao kwa hapa nchini hawafahamu umuhimu wake mwili licha ya kuwa wanauona tu katika mazingira wanayoishi.

Anasema kuwa ndani ya uyoga kuna virutubisho muhimu Uyoga una vitamini na aina nyingi za madini, Virutubisho vilivyothibitishwa kuwemo kwenye uyoga ni pamoja na Vitamin B2, B3, B5, B6,  pamoja na madini ya ‘Potasiamu’ na ‘Phosphorus’ amabayo ni muhimu mwilini katika kukinga na maradhi.

Anaendelea kwa kusema kuwa uyoga ni chanzo kingine kizuri sana cha madini ya chuma (iron) na kopa ambayo yanahusika kwa kiasi kikubwa na usambazaji wa hewa ya oksijeni mwilini.


“Vitamin B3 husaidia kupunguza kiwango cha mafuta mabaya ya lehemu mwilini, wakati Vitamin B6 yenyewe huondoa hatari ya mtu kupatwa na magonjwa ya moyo (heart attack) na Kiharusi au moyo kusimama kutokufanya kazi mwilini” alisema mtalaamu huyo.

Pia aliendelea kufafanua na kusema kuwa ndani ya mmea huo kuna madini ya zinki ambayo ni muhimu sana mwilini katika  kusaidia kinga mwili kupambana na vimelea vya magonjwa  na kuondoa seli zilizokufa katika mwili.

Pia anasema kuwa madini hayo ya zinki ndani ya uyoga husaidia mwili katika kutibu vidonda kwa haraka, hivyo unapokula uyoga unaipa mwili kinga na kuhifadhi madini hayo ambayo hukaa mwilini kwa kulinda mwili.

Anashauri kuwa sio kila uyoga unaliwa, hasa wanaokula uyoga kutoka katika mapori usitumie uyoga, bila kujua umetokea wapi bali uliza kwa wazazi ama watu wazima wenye busara kuhusu aina ya uyoga unao liwa, na kwa baadhi ya jamii hutumika kama kitoweo....


Comments

Popular posts from this blog

faida ya pili pili manga mwilini katika kutibu magonjwa

UJI WA ULEZI HUIMARISHA KIWANGO CHA SUKARI KWENYE UBONGO

KIAZI KIKUU NI ZAIDI YA CHAKULA, INATIBU!!!!