JINSI SUKARI INAVYOATHIRI NGUVU ZA KIUME

JINSI SUKARI  INAVYOATHIRI  NGUVU ZA KIUME


Na James Zakayo


Ni dhahili kuwa maisha yetu ya kifahari yametufanya kuwa tunakula vyakula vyakutosha na vyenye mvuto wa macho  lakini vyakula hivi si vyote ni vya  kujenga mwili bali vinakuja na magonjwa mengi ndani yake yanayoharibu afya ya mwili.Mtalaam wa tiba lishe  Amani Ezekiel kutoka kituo cha "Focus about Tommorow"  kilichopo Misungwi  mkoani MWANZA kwa kutambua madhara yatokanayo na kula vyakula vyenye sukari nyingi kutoka viwandani na kuendelea kula vyakula hivi bila kuwa na kiasi  ni kuufungulia mwili kuanza kukumbwa na magonjwa kadha wa kadha.Mtalaam huyo anafafanua kwa kusema kuwa  afya kwa ujumla wake hutengenezwa na mwenye mwili mwenyewe kwa kuruhusu nini kingie mwilini na kipi kisingiee, ikiwa anaingiza chenye tija kwa ajiri ya ujenzi wa mwili atakuwa na afya tele lakini akingiza kisicho cha afya basi mwili lazima kuanza kutoa matokeo mabaya ikiwa ni pamoja na magonjwa.
“Baadhi ya madhara ya vyakula vyenye sukari nyingi ni pamoja na nguvu za kiume ambazo hadi sasa wapo wanaume ambao hawawezi kutungisha mimba kwa kukosa mbegu na uwezo wa kuzalisha kutokana na vyakula hivyo” alifafanua mtalaam huyo.Anaendelea kwa kusema kuwa kumekuwa na usemi kuwa upungufu wa nguvu za kiume unahusishwa sana na umri mkubwa kwa mtu, ni dhahiri kuwa kuzeeka ama umri mkubwa kwako sio chanzo cha wewe kupata upungufu wa nguvu za kiume na hutakiwi kuhusisha bali ni tabia yako inayo ambatana na ulaji wa vyakula na unywaji wa vinywaji vyenye sukari nyingi.“Baadhi ya tabia hizo  ni pamoja na unywaji pombe, uvutaji sigara, utumiaji wa madawa ya hospitali bila ushauri maalumu na pia utumiaji madawa ya hospitali pale unapotibu baadhi ya magonjwa kwa mfano dawa za kifafa, dawa za usingizi na dawa za dege dege, utumiaji wa madawa ya kulevya na kujichua kila siku” alisema mtalaam huyo.Mtalaam huyo anfafanua kuwa tumekuwa tukiishi mazingira ya kula vyakula vya sukari kila siku kwa mfano, ukiamka asubuhi unakula mikate, tafiti zinasema kuwa mkate una aina ya wanga iitwayo amylopectin A ambayo endapo ikimeng’enywa ni chanzo cha sukari nyingi sana kwenye damu.Pia mtalaam huyo anaendelea kwa kusema kuwa unatakiwa kufahamu kuwa slice mbili za mikate ni sawa kama umeramba vijiko viwili vya sukari ya mezani yani sukari nyeupe, hivyo mikate ni moja ya vyakula vyakuepuka sana kama unahitaji kuwa na afya njema na mwenye nguvu za kiume na uwezo wa kutungisha mimba.“Imekuwa ni kawaida baadhi ya watu wanaamka asubuhi na soda kwani hii ni ishara kuwa tayari umekuwa muathirika wa sukari mahususi kwenye soda kitu  ambacho huitwa ASPARTAME kimeisha kuaathiri na umekuwa tegemezi na vyakula vya sukari” anafafanua mtalaam Ezekiel.


Mbali na hayo mtalaam huyo anasema Aspartame ni kiambata mahususi kwenye vinywaji vya coka na hivyo kimewekwa humo ili kukufanya uwe na hamu ya kunywa soda mara kwa mara au kula vyakula vitamu vitamu. Kiini hiki huenda kwenye ubongo na kujishika kwenye vipokea taarifa yani receptors na kutoa taarifa ambazo zina angamiza mwili wako.Sukari inapozidi mwilini inasababisha uchovyaji wa insulin kwa wingi ambayo hupunguza kiasi cha testosterone ndani ya damu na hatimaye kupunguza nguvu na shauku ya tendo la ndoa.“Kulingana na utafiti uliofanywa kwa kutumia kipimo cha sukari kiitwacho ORAL GLUCOSE TORELANCE TEST(OGT) kilionesha kuwa wanaume wenye sukari nyingi kwenye mzunguko wa damu walionesha kiwango kidogo cha kichocheo cha nguvu za kiume kiitwacho testosterone ambacho hushughurika na sifa za kiume,kutengeneza mbegu za kiume na kuimarisha misuli bila kusahau nguvu za kiume” anafafanua.
Mtalaam huyo anasema ni dhahili kuwa ongezeko kubwa la wanaume ambao wana matatizo ya nguvu za kiume inasababishwa na ulaji na unywaji wa vyakula vyenye sukari nyingi. Hivyo basi ni dhahiri kuwa kama una tatizo hilo linaweza kukupelekea kukosa mtoto kwani hata manii ya kiume kutengenezwa kwake itakuwa ni kwa shida sana.
Anasema kuwa Pia vyakula vya sukari nyingi hupunguza kwa hali ya juu vichocheo vya kujenga mwili yani GROWTH HORMONE ambayo hutolewa na tezi ya pituitary wakati wa usingizi mzito. Kichocheo hiki cha kujenga mwili yani GROWTH HORMONE kinafanya kazi kubwa ya kutumia mafuta yaliyohifadhiwa kwa matumizi ya ziada, pia growth hormone huimarisha misuli ya mwili na kuimarisha nguvu za kiume.
Hivyo kupungua kwa kichocheo hiki husababisha mrundikano wa mafuta mabaya na kutengeneza nyama zembe yani BELLY FAT, kuongezeka uzito,kupata kizuizi cha insulin na hatimaye kisukari aina ya pili.
“Vyakula vya sukari nyingi hukufanya muda wote ujihisi umechoka na huna nguvu ya kufanya kazi yoyote na wengine hufikiria kuwa wanasumbuliwa na ugonjwa wa malaria. Hii ni kwa sababu sukari nyingi kupita kiasi inasababisha utoaji wa insulin kuongezeka ili kupunguza sukari hiyo na matokeo yake kusababisha njaa na shauku ya kula mara kwa mara kwa sababu ya kupungua kwa reptin hormone inayotolewa na seli za kuhifadhi mafuta” anafafanua mtalaam huyoMtalaam Amani  Ezekiel anasema sukari nyingi huzuia utengenezwaji wa kichocheo kiitwacho OREXIN ambacho husafirisha taarifa na kuongoza kitendo cha ulaji na kukufanya uwe na nguvu ya kuwa macho na kufanya kazi zako. Sasa orexin inapopungua inasababisha muda wote kukaa umechoka na unasinzia ovyo ovyo.Pia mtalaam huyo kwa kuongezea anasema kuwa sukari nyingi kwenye damu husababisha msongo wa mawazo sana na hatimaye kusababisha utolewaji wa vichocheo vya CORTISOL ambayo husababisha ulaji ovyo wa vyakula wa bila mpangilio, mtu kama huyu utakuta unakula pale pale baada ya muda mfupi tena njaa.
Hivyo ni jukumu lako kujua nini cha kufanya kama wewe bado ujafikia ku athiriwa na tatizo hili ni dhahili kubadili mfumo wa maisha na kukubali mabadiliko katika vyakula nini kiliwe na nini kisiliwe kitatufanya kuwa wenye afya tele na wenye maarifa.“Chakula cha mimea na matunda kinakuweka mbali na dawa hizi wapenda kwani tusipende kula vyakula vyenye nembo ya kuisha muda wake. Kwa Yule ambaye tayari ameshakubwa na tatizo hili kwa sababu ya matumizi ya sukari nyingi napenda kukuambia kuwa  chakula pekee ni tiba kabisa na kujiepusha na dawa za kila siku unazo nunua ambazo hazitibu tatizo” anafafnua.Anaendelea kwa kufafanua kuwa kama huwezi kupangilia chakula chako vizuri na namna ya kuondoa tatizo lako unaweza tumia virutubisho vinavyo ondoa tatizo na kurudi kuwa kijana, kwa kutumia tiba ya mimea ama lishe pekee.Hivyo ni jukumu letu kuhakikisha jamii inaepukana na magonjwa haya kwani tukifanya hivyo utamaduni huu wa kutumia vyakula vya kiwandani vyenye sukari nyingi na madhara mengine mengi.Kuna msemo unasema kinga ni bora kuliko tiba hivyo kupitia hapa, mtalaam wa lishe anashauri kuwa huenda msomaji ni miongoni mwa waathiriwa wa sukari nyingi kwani uzito umekuzidi,kitambi,unasinzia ovyo ovyo na muda wote umechoka njia pekee ya kuachana na madhara  ya vyakula vya sukari ni kula  matunda na mboga mboga ndio suluhisho la afya yako.

kwa maoni na ushauri 
0719487615
jameszakayo36@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

faida ya pili pili manga mwilini katika kutibu magonjwa

UJI WA ULEZI HUIMARISHA KIWANGO CHA SUKARI KWENYE UBONGO

KIAZI KIKUU NI ZAIDI YA CHAKULA, INATIBU!!!!