MGAGANI HUPUNGUZA MAUMIVU YA UCHUNGU KWA MAMA MJAMZITO




Na James Zakayo 
                 MIAKA ya nyuma mboga ya asili ya majani aina ya mgagani haikuwa ikifahamika na watu wengi kwasababu mbalimbali, ilikuwa ikiota yenyewe porini na kwenye mashamba ambayo yalitekelezwa au kutolimwa muda mrefu.
Mboga hii pamoja ile ya mchunga hazikupendwa ukilinganisha na mboga zingine za majani kwasababu ya ladha yake kuwa chungu hivyo mapishi yake kuhitaji maandalizi marefu na kutumia muda mwingi.
 Kwasababu hizo, ilikuwa siyo rahisi kwa wakati huo  watu wa bara la Afrika ikiwamo Tanzania ambao ndio walaji wengi kutojua faida zingine za mboga hiyo kiafya.
Ni siku za hivi karibuni baada ya kukua kwa sayansi ya mimea na matokeo ya tafiti kuhusu mimea-dawa, mgagani umeanza kufahamika na watu wengi na sasa watu  huoteshwa kwa matumizi kama mboga na dawa hasa vijijini.
Dk. Edger Kapagi  wa kliniki ya bidhaa na dawa za asili inayojulikana kama Mazinmgira ya Jijini Mbeya, pamoja na faida zake lukuki katika afya ya binadamu, bado watu wengi hawaitumii kwa kuuita mboga ya watu masikini na pia kutoelimishwa na kujua umuhimu wake.
Anasema watafiti wamebaini kuwa mgagani unotambulika kwa jina la kibotania kama cleome gynandra ni kinga na tiba ya magonjwa mbalimbali kama vile  kisukari, saratani na magonjwa ya moyo. Mengine ni tiba ya maumivu ya kichwa, kufunga choo, maumivu ya tumbo, homa ya manjano (pneumonia), maumivu ya sikio, bawasiri, maumivu ya hedhi kwa wanawake kwa ulaji wa mara kwa mara kwa wanawake, hupunguza  uwezekano wa kupata uvimbe wa kizazi, jongo (gout), anemia na kuzuia kutapika. 
Kwa wajawazito wanaotaka kujifungua hurahisisha uzazi na kupunguza maumivu, kuongeza nguvu mwilini, kutoka maziwa kwa wingi kwa anayenyonyesha.
“Mgagani una virutubisho vya kutosha na madini kama vile beta carotene, vitamin C, Chuma, Magneziamu,  kalishiamu na fosforasi , protini na asidi nyingi aina ya  amino ambazo kwa pamoja ni muhimu mwilini, ” alisema Dk. Kapagi na kuongeza…
Mizizi hutibu homa, kuumwa na nge na nyoka. Lakini ni mboga nzuri kwa waliotoka tohara kwani huongeza damu haraka iliyotoka wakati wa kutahiriwa.
Ni mboga nzuri kwa watoto kwani inaupunguza mtoto kukubwa na baadhi ya magonjwa nyemelezi na ili kupunguza uchungu changanya na tui la karanga kupunguza uchungu ili mtoto aweze kula bila shida, alisema.

Kwa mujibu wa Dk.Kapagi mbegu za mgagani  zinaweza kukamuliwa na kusafishwa ambapo mafuta yake hutumika kutengeneza sabuni na vitu vingine.
 Majani na mbegu ni chakula kizuri cha kuku na ndege wengine pamoja na wanyama kama vile ng’ombe, ngamia, farasi na wengine wanaofugwa, alisema.

Akifafanua , anasema mgagani husadikiwa kuwa asili yake ni Afrika mashariki, Ethiopia, Somalia, Asia Kusini na Amerika, kwa sasa imeenea katika nchi zote zenye hali ya kitropiki  barani Afrika, Asia na Amerika. Barani Asia walaji wakubwa wa mboga hiyo ni  wahindi na watu wa kabila la wathai (Thailand), huutumia kama mboga na dawa.

Comments

Popular posts from this blog

faida ya pili pili manga mwilini katika kutibu magonjwa

UJI WA ULEZI HUIMARISHA KIWANGO CHA SUKARI KWENYE UBONGO

KIAZI KIKUU NI ZAIDI YA CHAKULA, INATIBU!!!!