UFUTA HUTIBU KISUKARI , SARATANI, `PRESHA’



Na James Zakayo 
                       TAKWIMU zinaonesha kuwa zao la ufuta huiingizia serikali fedha nyingi ambapo  asilimia 32 ya pato la taifa hutokana na mauzo ya zao hilo la mbegu.
Ufuta au sesame hujulikana kwa lugha ya kisayansi kama Sesamum indicum,  hustawi na hulimwa zaidi mikoa ya kusini mwa Tanzania ya Lindi, Mtwara na sehemu ya mkoa wa Ruvuma, Tunduru.
Pia hulimwa kwa uchache kwenye maeneo mengine ya nchi yenye ukanda wa joto. Wilaya za Liwale na Ruangwa mkoani Lindi hasa kata ya Nanjilinji zinatajwa kulima kwa wingi zao hilo.
Walaji hulitumia kama kipooza njaa kwa kutafuna kama karanga, pia husindika mbegu hizo na kupata mafuta ya kupikia. Kwa bahati mbaya sana ni kwamba wengi wanaotumia hawatambui faida zingine za ulaji wa ufuta kiafya zaidi ya kulitumia kama lishe pekee.
Hata hivyo, tafiti mbalimbali za ndani na nje ya nchi,  zinaonesha kuwa ulaji wake ni kinga na tiba ya magonjwa katika mwili wa binadamu.
Baadhi ya magonjwa hayo ni kisukari, shambulio la moyo, kuimarisha mmengenyo wa chakula, huondoa lehemu, huboresha ngozi, huondoa na kukinga saratani na  kuongeza damu.
Pia ufuta  huzuia mwili kuharibiwa na mionzi na mionzi ya jua, hulinda ini dhidi ya madhara ya pombe, hung’arisha ngozi  na kuimarisha afya ya macho.
Dk. Raphael Nyampiga ni mtaalamu wa tiba lishe katika kituo cha huduma hiyo kilichopo Pugu nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, anataja faida zingine kuwa ni kuzuia maradhi ya kinywa.
Pia  huimarisha mfumo wa upumuaji, lishe kwa watoto wadogo na kuimarisha afya ya nywele na hivyo kuzuia tatizo la nywele kunyonyoka na kuota nywele kwa wale wenye uhaba au kutoota nywele.
Hiyo ni kutokana na aina mbalimbali za virutubisho vilivyomo katika mbegu za ufuta kama vile, protini,  mafuta, madini kadhaa kama ya kopa, kalishiamu (calcium), chuma, zinki, fosforasi, manganizi, magineziamu na thiamine.

KISUKARI:

Huzuia na kutibu ugonjwa huo  kutokana na mbegu zake kuwa na madini ya magneziamu ambayo yakiwa mwilini huzuia visababishi vya sukari kama vile tatizo la insulini na kongosho kutofanya kazi ipasavyo.
Pia  mafuta ya ufuta huimarisha kuta za plasma na hatimaye kuwa na uwezo zaidi wa kuweka sawa kiwango cha sukari kwenye damu, alisema.

         KUKOSA CHOO, SARATANI, KINYWA:

Dk. Nyampiga anaongeza kwa kusema kuwa, mtu mwenye matatizo ya kukosa choo au choo kigumu, anapaswa kula kwa wingi ufuta kutokana na virutubisho hivyo kurahisisha mmeng’enyo wa chakula na kufanya hali hizo kutoweka na kuondokana na tatizo la ugonjwa wa bawasiri.
Kuhusu  ugonjwa wa Saratani, anaongeza kwa kusema kuwa mbegu za ufuta zina misombo (compounds) kama vile asidi aina ya phytic  madini ya maginesiamu na phytosterols  ambayo kwa pamoja huukinga  mwili na kundoa sumusumu zinasababisha saratani.
 “Ufuta pia ni  tiba ya matatizo yanayokabili kinywa. Kwa miaka mingi sasa watu wa jamii la kabila la Ayurveda huko barani Asia, wamekuwa wakitumia mafuta ya ufuta kama tiba na kinga ya matatizo ya kinywa ikijumuisha meno, fizi na kingo za  mdomo au kinywa,”alisema Dk. Nyampiga.
                
 SHINIKIZO LA DAMU (PRESHA), MATATIZO YA UZAZI, KUONDOA KITAMBI:

Naye Dk. Zawadi Abdallah wa kituo cha dawa asili cha  Zawadi Herbarist  cha Tabata jijini hapa, anasema ufuta hutibu matatizo ya  moyo na shinikizo la juu la damu (presha ya kupanda) ambapo mara baada ya kula ufuta hushuka na kuwa la wastani kwa muda mfupi ikiwa matumizi yake yatazingatiwa.
“Ufuta huweza kuimarisha moyo na kuulinda  usishambuliwe na  magonjwa ikiwa ni pamoja na kushusha `presha’ ya juu kutokana na virutubisho  hivyo,”alisema.
Pia kiwango protini cha kiasi cha gramu 4.7 kilichomo ni lishe muhimu kwa watoto wadogo kutokana na virutubisho na misombo hiyo kusaidia kuimarisha afya ya mtoto, kukua haraka na kumkinga dhidi ya magonjwa.
Zaidi anasema, unapoliwa kwa wingi hufanya kazi  muhimu ya kuzibua mirija ya uzazi kwa jinsia zote,  kuimarisha na kuboresha mbegu za kiume, hali ambazo kwanzo huruhusu mwanamke kushika mimba au mwanamume kuwa na uwezo kutungisha mimba.
Anafafanua zaidi: Mafuta ya ufuta ni mazuri kwa afya ya mwili kwa kuwa yametokanana na mbegu za ufuta, hivyo yakitumiwa kwa kuzingatia ushauri, huondoa mafuta mabaya (lehemu) mwilini na kubaki na mafuta yanayohitajika hivyo kuondokana na tatizo la kitambi na madhara mengine ya moyo.
Pia mafuta haya husaidia kuimarisha afya, ngozi ya mwili kung’aa na mtu kuwa na muonekeano mzuri na wa kuvutia, alisema.

MATATIZO YA FIGO, KIBOFU:

Nao utafiti wa Dk. Kurian ambao matokeo yake aliyachapisha katika kitabu chake kinachojulikana kama Healing Wonders, anasema kwa  ujumla zao la ufuta ni tiba muhimu katika tiba ya figo ikiwamo kuondoa  mawe kwenye figo na matatizo ya kibofu.
Pia una uwezo wa kutibu kipindupindu na kuzuia kuhara, kuweka sawa homoni zinazosababisha mzunguko wa hedhi kwa mwanamke kwenda sawa, alisema na kuendelea…
Huongeza nguvu kwenye mifupa na kuimarisha misuli mwilini kutokana na  kirutubisho cha Kalishiamu kilichomo. Unazuia na kutibu maumivu ya  tumbo ya ghafla.
“Ufuta pia ni tiba nzuri kwa matatizo ya mfumo wa upumuaji kwani virutubisho vilivyomo huyakinga mapafu dhidi ya hewa chafu na magonjwa yanayoambata na kusababisha mfumo wa hewa kutokuwa mzuri,”alisema Dk. Kuria.

MATATIZO YA INI NA MACHO:

Mtaalamu mwingine wa tiba lishe,   Dk. Josh Axe  wa nchini Marekani anasema kupitia kitabu chake cha Eat Dirt kuwa ufuta hulinda ini dhidi ya magonjwa.
Hiyo ni pamoja na  kulifanya ini  kuwa na uwezo wa kufanya kazi ipasavo na kuliepusha na magonjwa hasa ikiwa  limeathiriwa na pombe kwani ufuta huondoa sumusumu zilizomo zinazotokana na matumizi ya pombe.
Katika nchi za Asia ikiwamo China na India, ufuta  umekuwa ukitumika kama tiba ya watu wenye matatizo ya macho hasa ufuta wenye rangi nyeusi. Huu husaidia pia ini, hivyo upo uhusiano mkubwa kati ya ini na macho katika kutibiwa na ufuta, alisema Dk. Axe.
“Tumetafiti na kufanya majaribio kwa watu kadhaa na kugundua kwamba hung’arisha ngozi na kuzuia athari zitokanazo na mionzi ya jua kupenya katika mwili kutokana na kiwango cha mafuta yake, kwamba hulinda ngozi ya mwili na kuepusha na saratani inayosababishwa na mionzi jua, kuongeza damu na kuondoa sumusumu za kemikali hasa kutoka kwenye pombe na vinywaji vingine vya kaboni laini,”alisema.

NYWELE KUTOOTA NA KUNYONYOKA:

Dk. Nyampiga anaongeza kwa kusema kuwa ufuta ukitumiwa vizuri na kwa usahihi pia huimarisha nywele na afya ya kichwa,  hivyo kuwafanya watu wenye matatizo ya kutoota  nywele na nywele kunyonyoka kuondokana na madhila hayo.

NAMNA YA KUTUMIA KWA NIA YA TIBA, KINGA:

Kwa mtu mwenye umri kuanzia miaka 12 na kuendelea, wataalamu hao wanashauri mhusika kusaga ufuta kisha kijiko kimoja cha chai cha unga huo kuchanganya kwenye chai, uji au supu iliyomo kwenye kikombe au bakuli vya wastani.
Mhusika anashauriwa kunywa mchanganyiko huo kwa dozi ya mara mbili kwa siku (kwa mfano asubuhi na jioni) yaani kila baada ya masaa nane katika  kipindi cha mwezi moja au zaidi kulingana na ukubwa wa tatizo.
Kwa watu wa chini ya umri wa miaka 12 wanashauriwa kuchanganya nusu kijiko cha chai cha unga wa ufuta uliosangwa kwenye chai, uji au supu cha ujazo wa wastani katika kikombe au bakuli. “Tumia mchanganyiko huo kwa kunywa mara mbili kwa siku kwa muda wa siku 14  au zaidi kulingana na ukubwa wa tatizo husika,”imeshauriwa.
==================



Comments

Popular posts from this blog

faida ya pili pili manga mwilini katika kutibu magonjwa

UJI WA ULEZI HUIMARISHA KIWANGO CHA SUKARI KWENYE UBONGO

KIAZI KIKUU NI ZAIDI YA CHAKULA, INATIBU!!!!