KIAZI KIKUU NI ZAIDI YA CHAKULA, INATIBU!!!!
Kiboko ya
kisukari, `gono’, ukoma
Hutibu bawasiri, matatizo ya hedhi, moyo
Na James Zakayo
Ni
mmea unaotambaa kwa msaada wa mti mithili ya
mmea mwingine maarufu wa mpensheni, lakini tofauti yake ni kwamba mizizi yake hunenepa na kutambaa chini ya
ardhi kama ilivyo muhogo au viazi vitamu na mizizi hiyo huitwa viazi vikuu.
Dk. Raphael Nyampiga ni mtaalamu wa miti na mimea dawa kutoka
kliniki ya miti na mimea dawa inayojulikana kama Atukuzwe ya Pugu Jijini Dar es
Salam, anasema mmea huo huweza kuwa na urefu wa zaidi ya mita moja na kwamba kiazi kimoja
hufikia uzito wa hadi kilogramu 50 kulingana na eneo ulimopandwa.
Katika mahojiano na TABIBU
hivi karibuni, Dk. Nyampiga anasema hata hivyo
misombo (compounds) zilizomo kwenye kiazi husaidia kupambana na sumusumu mwilini
hasa kwenye kongosho, shambulio la moyo, bawasiri na huondoa uzito uliopitiliza
mwilini na kitambi.
“Tangu
zamani kiazi kikuu kilifahamika kama tiba ya matatizo ya mfumo wa mmeng’enyo wa
chakula na tiba ya bawasiri. Hii ni kwa sababu kina wingi wa kamba lishe na
misombo inayotibu ugonjwa huo,”alisema.
Faida
zingine za kiafya za kiazi kikuu, Dk. Nyampiga anasema kuwa ni miongoni mwa
vyakula vinavyosaidia kusafisha damu na
kuondoa vikwazo katika mishipa ya damu vinavyozuia damu kuzunguka mwili.
Pia
kamba lishe hizo zina uwezo wa kurekebisha kiwango cha sukari mwilini, matatizo
ya hedhi na kuweka sawa mfumo wa homoni za uzazi kwa mwanamke.
Husaidia kuondoa muingiliano wa homoni zinazovuruga mfumo wa
hedhi na huongeza kuzaliana kwa homoni
inayochochea uzalishwaji wa mayai kwa mwanamke, alisema.
Kwa
wasichana wanao karibia umri wa kuvunja ungo (kupevuka), wanashauriwa na
mtaalamu huyo kula kwa wingi kiazi kikuu kwani kinapoliwa katika umri huo husaidia zaidi
kuweka sawa homoni zao katika mwili pindi watakapoanza mzunguko wa hedhi.
Kwa upande mwingine, tafiti za nje ya Tanzania kuhusu tiba
inayotokana na kiazi kikuu, Dk. Kurian katika kitabu chake cha Healing Wonders of Plants anasema pamoja
na kutibu maradhi yanayotajwa na Dk. Nyampiga, pia hutibu ukoma.
Zaidi, anaainisha
katika utafiti wake kuwapo kwa virutubisho kadhaa kwenye kiazi kikuu kama vile protini,
mafuta, wanga, sukari na kamba lishe. Pia vitamini vya thiamini, riboflavini,
niazini na folate.
Virutubisho
vingine kwenye kiazi kikuu ni madini ya magneziamu, kalisiamu,
chuma, fosforasi, potaziamu, sodiamu, zinki, kopa, seleniamu, manganizi, misombo ya beta-karotini, folikiloriki na pantotheniki ambavyo kuwapo
kwake mwilini husaidia kupambana na maradhi hayo.
Pia
hutibu ugonjwa wa zinaa aina ya kisonono maarufu kwa vijana wengi kama `gono’
ambao ni kifupisho cha neno la kitaalamu la gonorrhea,
kabla haujakomaa mwilini.
“Ili
kuweza kuondoa na kupunguza sumusumu na magonjwa katika mwili wa binadamu, lazima tukubali na kuheshimu vyakula vya asili
na ambavyo havikusindikwa na
kuchanganywa na kemikali,” alisema.
Nao,
utafiti uliofanywa na ripoti yake kuchapishwa katika jarida la Philippine Journal of Science , unaibainisha kuwa, kiazi kikuu
ni chanzo cha vitamini B6, ambayo husambaratisha kemikali hatari kama vile homocysteine.
Kemikali
hiyo, huathiri mishipa ya damu na kuzuia
damu kutofika sehemu zote za mwili hivyo kusababisha tatizo la shambulio la moyo, sehemu ya
utafiti huo imeonesha.
MATUMIZI:
Dk.
Kurian anashauri kuwa ili kutibu magonjwa hayo, mhusika anatakiwa kukatakata kiazi kikuu
vipande vidogo vidogo, kuvichemsha kwa muda wa dakika 20 hadi 30, kisha kula kwa
kadri ya uwezo wake. Inashauriwa kula mlo
huo mara kwa mara.
“Ni
muhimu kunywa supu ya viazi vilivyopikwa
wakati wa kula mlo huu kwani supu hiyo imebeba mchangnyiko wa virutumisho hivyo
,”alisisitiza.
Naye
Dk. Nyampiga: “Kiazi kikuu kinaweza kumenywa na kukaushwa juani, kusagwa kama
ilivyo muhogo. Mgonjwa wa kisukari au mhudumu wake achanganye unga wa kiazi kikuu kiasi cha
nusu kijiko kidogo na maji ya moto katika ujazo wa kikombe cha chai, kisha kunywa kwa dozi ya kutwa mara mbili, kwa
mfano asubuhi na jioni, ”alifafanua.
==============
Comments
Post a Comment