UJI WA ULEZI HUIMARISHA KIWANGO CHA SUKARI KWENYE UBONGO
Na James Zakayo
WATU
wengi katika jamii huamini na kutumia chai kama kifungua kinywa. Yamekuwa
mazoezi enzi na enzi. Bahati mbaya sana ni kwamba watu wengi hufungua kinywa
bila malengo.
Katika
hali hiyo, Dk. Raphael Nyampiga wa kituo cha tiba lishe cha Atukuzwe chenye
makao yake, Pugu nje kidogo ya Jijini la Dar es Salaam anasema ni muhimu jamii
kutambua ni kifungua kinywa gani ni sahihi na kupata kiburudisho hicho kwa
malengo.
Zaidi,
mtaalamu huyo anasema katika kutambua usahihi na malengo ya kifungua kinywa ni
muhimu pia kutambua umuhimu wa lishe bora, kunywa au kula kwa muda gani na kipi
kiliwe na kwa muda upi kulingana na aina
hizo za chakula ikiwamo kifungua kinywa hasa uji wa ulezi.
Anasema
uji wa ulezi ni miongoni mwa vyakula muhimu
katika afya ya binadamu, yafaa jamii kukitumia kwa wingi zaidi kama
kifungua kinywa, kulingana sifa zake mwilini na virutubisho vilivyomo.
“Unapokunywa uji wa ulezi asubuhi kama
kifungua kinywa mara baada tu ya kutoka kitandani kabla ya kula kitu chochote
huchukua nafasi kubwa sana ya kufanya siku yako kuwa bora zaidi katika majukumu
yako ya siku nzima”alisema Dk. Nyampiga na kuendelea...
“Kifungua kinywa hiki pia kinawawezesha wanafunzi kufaulu vizuri mitihani yao na kupata
alama za juu kwa mitihani waliyofanya
kabla ya mapumziko yao ya mchana…nguvu hizo zinazotokana na kifungua kinywa cha
uji wa ulezi zimeimarisha kiwango chao cha sukari kwenye ubongo, na zimeimarisha
uwezo wa kufikiri, pia kuwa wasikivu.” alisema.
Pia
alisema kuwa ndani ya uji wa ulezi kuna virutubisho muhimu vya kuifanya akili
kufanya kazi ya kuwa na kumbukumbu na mwili kuwa na nguvu kubwa katika kumfanya
mtoto awe na ari ya kujisomea ndio maana hata mama wajawazito wanashauriwa
kunywa uji wa ulezi mara baada ya kujifungua ili kurudisha nguvu.
“Wakati
wa miaka 70 tulikuwa tunashindia uji wa ulezi kutokana na virutubisho vilivyomo
ndani yake kwa kuwa vilitupatia nguvu kubwa ya kuufanya mwili kuwa na nguvu ya
ziada kwa muda mrefu , lakini kwa kuwa sasa
hivi watoto wetu wengi hawapewi uji wa ulezi asubuhi hivyo hawawezi kuwa
na uvumilivu wa kushinda muda mrefu bila kula” alisema.
Kwa
kuunga mkono hoja hizo naye Dk. Raymond Shirikisho kutoka KCMC alisema kuwa
mwili wa binadamu unafanya kazi kama mashine hivyo kama kuna kifaa hakina
mafuta muhimu na ya kutosha basi si rahisi msuguano kutokea ili mashine ifanye
kazi, hivyo unywaji wa kifungua kinywa asubuhi na mapema unapoamka ni muhimu
kwa afya ya akili.
“Unywaji
wa uji wa ulezi ni muhimu pale unapoamka kwa kuwa unafungua akili ili iweze
kufanya kazi katika kiwango cha juu
tofauti na wale wasiokunywa kifuangua kinywa cha aina yoyote”alisema Dk.
Shirikisho.
Walitoa
wito kwa jamii kurudi katika kula vyakula vya asili na kuachana na vyakula
visivyo na tija katika mwili wa binadamu. “Wazazi wanaaswa kuwandalia watoto
wao uji wa ulezi asubuhi na mapema kabla hawajatoka kwenda shuleni ili kuweza
kufungua akili ya mtoto na kuwajengea uwezo mkubwa wa kufikiri,”alisema
Nyampiga.
Comments
Post a Comment