MCHANGANYIKO WENYE TIBA NA KINGA YA MAGONJWA





Na. James zakayo

Vipo baadhi ya vyakula ambavyo hutumiwa na binadamu bila wao kujua kuwa vyakula hivyo ni faida kubwa kiafya, kwa kuwa vina uwezo wa kuzuia na kutibu baadhi ya magonjwa mwilini.
Miongoni mwa mimea hiyo ni tunda la embe na parachichi, mchanganyiko wake umethibitika na tafiti mbalimbali kuwa ina uwezo wa kutibu magonjwa katika mwili, embe hujulikana kwa jina la kisayansi Mangifera indica huku kwa jina la kingereza kama mango na parachichi hujulikana kisayansi kama Persea americana na kwa jina la kingereza kama Avocado.
Tafiti mbalimbali kutoka ndani na nje zimelezea kuwa mchanganyiko wa juice hii inatibu na kukinga magonjwa mbali mbali ikiwamo magonjwa ya moyo, kuondoa mawe kwenye figo,matatizo ya macho, kuongeza kinga ya mwili na kuondoa lehemu mwilini.
Pia tafiti hizo zimelezea kuwa mbali na hayo pia juisi hii huimarisha misuli, hutibu saratani, huzuia harufu mbaya mdomoni, kuzuia makali ya vidonda vya tumbo, kuongeza urembo kwenye ngozi na kuondoa uchovu kwa mama wajawazito wanapoamka asubuhi.
Ugonjwa wa moyo.
Dk. Geoffrey Lusanzu kutoka Salem kliniki ilioko Kasulu Kigoma ameliambia gazeti hili kuwa mchanganyiko wa juisi hii ya embe na parachichi ni neema kwa wenye matatizo ya moyo (Blood pressure) kwa kuwa ndani ya mchanganyiko huo kuna wingi wa kamba lishe na misombo (compounds) muhimu kwa ajiri ya kuzuia visababishi vya ugonjwa wa moyo.
“Ndani ya mchanganyiko wa juisi hii kuna kamba lishe ambazo huingia mwilini na kusafisha mishipa ya damu na kuifanya damu kusafiri bila kizuizi chochote” alisema Dk. Lusanzu.
Akiendelea kufafanua alisema kuwa misombo ilioko ndani ya mchanganyiko wa juisi hii huusaidia mwili katika kuondokana na mafuta kujaa katika mishipa ya damu , kwa kuwa mafuta huzuia damu kusafiri hivyo matumizi sahihi ya  mchanganyiko huu husaidia kuondokana na tatizo hilo.
Naye Dk. George Pamplona katika kitabu chake cha Health Food anasema kuwa ndani ya embe na parachichi kuna madini ya sodium na potassium ambayo ni muhimu kwa kuzuia matatizo ya moyo.
Kwa kuunga mkono hoja hizo Dk. Rafael Nyampiga kutoka Atukuzwe kliniki ilioko Pugu jijini Dar es saalam ameliambia Gazeti hili kuwa miongoni mwa tiba na kinga nzuri iliyosaulika ni matumizi ya juisi katika kuzuia magonjwa yanayokabili moyo, miongoni mwa juisi hizo ni mchanganyiko wa embe na parachichi.
Ugonjwa wa saratani
Mwandishi  Dk. Kurian katika kitabu chake cha healing wonders of plant amelezea kuwa  ndani ya matunda haya mawili kuna misombo(compounds) ambazo hufanya kazi kubwa mwilini ya kuondoa sumu sumu zenye kuweza kusababisha kutokea kwa saratani.
“Misombo iliyomo ndani ya mchanganyiko wa matunda haya husaidia mwili katika kuondoa chembe chembe za saratani mwilini” amesema Dk. Kurian.
Akiendelea kufafanua alisema kuwa miongoni mwa saratani zinazoweza kuzuiliwa na kutibiwa na mchanganyiko wa matunda haya ni saratani ya tezi dume(prostate) saratani ya matiti.
Naye Dk. Rafael Nyampiga alifafanua kuwa ndani ya juisi hii kuna kuna virutubisho vya pekee vijulikanavyo kitalaamu kama phytonutrient  ambazo huzuia saratani mwilini na kuondoa chembe chembe za saratani.
Akiendelea kufafanua Dk. Nyampiga anasema kuwa  ndani ya mwili wa binadamu umeumbwa kuingiza baadhi ya vyakula ambavyo husaidia mwili kukua hivyo, saratani hutokana na kula vyakula visivyo na ulazima hivyo juisi hii itasaidia kuondokana na sumu zinazosababisha saratani hizo.
Nuru ya macho.
Dk. Lusanzu katika utafiti wake aliliambia gazeti hili kuwa mchanganyiko wa juisi hii ni muhimu sana katika tiba ya matatizo ya uonefu hafifu na kuimarisha nuru ya macho.
“Mchanganyiko wa juisi hii ya parachichi na embe ni vyakula muhimu katika kuimarisha nuru ya macho hasa kwa wazee ambao wanakabiliwa na changamoto ya nuru ya macho”aliongezea Dk. Lusanzu.
Pia tafiti kutoka katika mtandao wa www.dr.health unaeleza kuwa juisi hii huimarisha misuli ya macho iliyolegea na kuimarisha macho hasa kwa umri wa watu wazima na wale wenye matatizo ya macho.
Kuondoa mawe kwenye figo.


Katika kuondoa mawe kwenye figo Dk. Nyampiga anaelezea kuwa juisi hii husaidia kuondoa mkusanyiko wa uchafu ndani ya figo unaoleta mawe ya figo na kuyayeyusha na kutolewa nje.
“Juisi hii ikizingatiwa kwa vipimo sahihi ina uwezo wa kuondoa mawe katika figo na kuondokana na madhara yatokanayo na mawe kwenye figo ikiwa ni pamoja na maumivu makali ya nyonga na tumbo” aliongezea Dk. Nyampiga.
Naye Dk. Pamplona ameongezea kuwa mchanganyiko wa juisi ya parachichi ina virutuibisho muhimu kwa ajili ya kuyeyusha mawe yalio ganda kwenye figo na kuleta matatizo mwilini.
Kuongeza kinga mwili.
Katika kuongeza kinga ya mwili Dk. Lusanzu anasema kuwa juisi hii ni maarufu katika kuondoa sumu sumu mwilini zinazoingia kwa njia ya chakula ama kwa njia ya hewa, katika kuzungumzia hili “ ndani ya mchanganyiko wa chakula chochote chenye embe na parachichi kuna misombo muhimu inayohusika kuondoa sumu katika mwili” ameongezea Dk. Lusanzu.
Akiendelea kufafanua Dk. Lusanzu anasema kuwa  matunda haya mawili yanauwezo wa kuongeza kinga ya mwili kwa asilimia kubwa kuliko aina nyingine ya matunda kwani ina aina nyingi za virutubisho.
Naye Dk. Nyampiga ameliambia gazeti hili kuwa miongoni mwa matunda maarufu kwa kuongeza kinga ya mwili na kufanya mwili kuwa imara ni pamoja na tunda la parachichi hivyo mchanganyiko ulio na hili tunda ni muhimu kwa afya na kujenga mwili na kinga.
 Kuondoa lehemu mwilini.
Katika kuzungumzia juu ya faida ya juisi ya mchanganyiko huu katika tiba  Dk. Nyampiga alisema kuwa parachichi lina mafuta mazuri ambayo yakingia mwilini hufanya kazi ya kuondoa mafuta mabaya (cholesterol) mwilini.
“Parachichi lina mafuta mengi na muhimu kwa mwili, mafuta ya parachichi yenyewe ni dawa mwilini hivyo ikichanganywa na kambalishe za embe ni tiba tosha kwa kuondoa lehemu” alisema Dk. Nyampiga.
Pia aliongezea kwa kusema kuwa juisi hii hufanya kazi ya kuboresha ngozi, na kuonda mabaka na kuzuia athari zitiokanazo na mionzi ya jua na kuifanya ngozi kuwa yenye urembo na mng’ao unaovutia.
Akiendelea kufafanua  alisema kuwa pia huimarisha ngozi ya kichwa ili kuruhusu uotaji wa nywele na huzuia kuota kwa vipara na hujaza wingi wa nywele katika kichwa na kuzifanya kuwa na afya, na kuzuia kukatika katika.
Dk. Lusanzu anasema kuwa juisi hii ni muhimu mwilini kwa kuwa hupambana na asidi kali zinazosababisha watu wenye vidonda vya tumbo tumbo kuwaka moto, pia husaidia kuzalisha ute ute unaosaidia kuondoa vidonda vya tumbo.
“Pia ni tiba kwa wale wenye matatizo ya kutokwa na harufu mdomoni kwa kuwa ina harufu nzuri na huondoa kunuka kwa kinywa” amesema Lusanzu.
Dk. Nyampiga anasema kuwa ni tiba na kinga kwa mama wajawazito wale ambao wanamka asubuhi wakiwa na uchovu, husaidia kuzuia kutapika kwa mama mjamzito ikiwa atakuwa anakunywa mara kwa mara wakati wa ujauzito, pia ina kirutubisho cha folate muhimu kwa mama hao katika kuzuia watoto kuzaliwa na ugonjwa wa mgongo wazi na vichwa maji.
Jinsi ya kutumia  
Chukua parachichi moja na embe moja menya katakata changanya nusu glasi ya maji saga kwa pamoja kunywa juisi hiyo glasi moja asubuhi na glasi moja jioni kwa muda wote kadri uwezavyo maana pia ni chakula.

KWA MAONI 
0719487615
jameszakayo36@gmail.com     


Comments

Popular posts from this blog

faida ya pili pili manga mwilini katika kutibu magonjwa

UJI WA ULEZI HUIMARISHA KIWANGO CHA SUKARI KWENYE UBONGO

KIAZI KIKUU NI ZAIDI YA CHAKULA, INATIBU!!!!